Showing posts with label KIDUM. Show all posts
Showing posts with label KIDUM. Show all posts

Wednesday, 13 July 2016

MULIKA MWIZI LYRICS BY KIDUM FT SANAIPEI


Verse 1

Ukiona mwanaume kwa hali ya kulia, jua yakwamba ameguswa pahali

Sio rahisi, si kawaida kushuhudia mwanaume akitoa machozi

Hapo zamani nilidhani mwanaume akipoteza kazi ndio uchungu, ndio unyonge 

Kumbe mapenzi ndio sumu kali, inayofanya mwanaume kulia

Kama mtoto mtoto, kama kidogoyo

Hapembelezwi, hanyamazishwi, machozi yake inatoka ikienda tumboni

Hapembelezwi, hanyamazishwi, machozi yake inatoka ikienda tumboni



Chorus

Mulika mwizi, mulika na tochi, mulika (mulika mwizi)

Mulika mwizi, kama kuna giza mulika

Nimulikie mwizi, nasumbuka, nataka kujua nani mwizi wa mapenzi

Barua pepe kwa simu ya rununu, ujumbe mfupi unafutwa na sekundi tatu (sekundi tatu)

Nilimpenda baibe wangu, nikampea roho yangu, amechukuliwa, amenyakuliwa

Jamaa fulani hapa mtaani, mwenye magari, na mapesa, amechukua baibe 

Ikanifanya crazy,sipembelezwi, sinyamazishwi
Machozi yangu yanatoka yakienda tumboni

Msiomboleze, mnamujua huyu jamaa, kajifanya bubu, wengine vipofo




Chorus

Mulika mwizi, nimulikie mwizi

Nimulikie mwizi, nasumbuka, nataka kujua nani mwizi wa mapenzi

Nani mwizi wa mapenzi



Verse 3

[Sanaipei]

Ukiona baibe wako anaingia bafu na simu mkononi, huyo ni mwizi (mulika mwizi)

Uniona mzee wako anazima simu kila mara akiwa kwa nyumba, mulika mwizi (mulika mwizi)
 Oh-o-o-o oh oh  oh-o-o-o
Oh-o-o-o –o-o


Nimulikie mwizi jameni, (mulika mwizi)

Mulika mwizi, nionyeshe, niambie ni wapi

Nimulikie mwizi, mwizi wa mapenzi, mwizi wa mapenzi (mulika mwizi)

Nani mwizi wa mapenzi

Nani mwizi wa mapenzi (mulika mwizi)

Wani ua, wani umiza (oh –o-o-o-o)

Mulika na tochi, natazama mbele si nyuma

Mulika mwizi, kila mtu mwizi wa mapenzi, kila mtu mwizi wa mapenzi


Pia mimi mwizi wa mapenzi

NITAFANYA LYRICS BY KIDUM


Verse 1 [Kidum]

Ikiwa umeamua kunitoroka

Ikiwa unahisi hujiskii nami tena

Na mbona imekuwa ngumu kunidokeza

Naona ni bora nilie leo, badala ya kesho

Kupenda, usipende Ni kama kujitia kitanzi

Nitachimba na sururu Kwa ardhi nikitafuta penzi lako

Ni heri nipigwe fimbo kwa mwili

Sababu ntajikuna ama ntajikanda na maji moto

Maumivu ya penzi, mtu hajikuni

Wala hajikandi na maji, na hakuna upasuaji



Chorus

Kama Kuna kosa nimewahi fanya (nielezee)

Kama Kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi)

Na kama Kuna kitendo linaweza tendwa (nielezee)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Verse 2 [Lady Jay Dee]

Kweli hukumbuki ulioyafanya Ni kweli unakumbuka tulikotoka

Sisemi habari zozote za kusikia Bali kwa ushahidi niliouona

Msamaha mara ngapi Umeshaomba na bado

Chenye makosa mangapi Niliyoyafumbia macho

Mpaka leo nahisi kufika kikomo Maumivu yanazidi

Ndani ya moyo Sitaki kwenda mbali kwani uko moyoni

Nikusamehe mimi mara ngapi wee Nielezee mpenzi mara ngapi

Chorus

Unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu)

Ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho)

Je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia) Sitoweza (utaweza wee)

Nimechoka (usichoke) Nimeshindwa (usishindwe)

Naondoka (usiondoke) Sitoweza (utaweza yee)

Nimechoka Nimeshindwa (usishindwe)

Naondoka (usishindwe)



Verse 3

Ukihesabu mara ngapi umenisamehe Ni kama kuhesabu 

Ni mara ngapi mtoto kaharibu nappy Usichoke

Usiondoke Usilie Niko hapa kukulinda

Chorus

Kama Kuna kosa nimewahi fanya (nielezee)

Kama Kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi)

Na kam Kuna kitendo lingeweza tendwa (nielezee)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu)

Ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho)

Je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia)

Sitoweza (utaweza wee) Nimechoka (usichoke)

Nimeshindwa (usishindwe) Naondoka (usiondoke)

Sitoweza (utaweza yee) Nimechoka

Nimeshindwa (usishindwe) Naondoka (usishindwe)

MAPENZI LYRICS BY KIDUM


verse 1

Kama ni mapenzi Ya kuniudhi kila saa

Ya kunifanya mi kulia Na kama huridhiki

Na mbona hujasema Ili niweze rekebisha

Nifanye mambo shwari Nikiamini u kwangu

Na kukusifu kwa wazazi Hujali tenda hisia zangu

Sijui tunapokwenda Lakini najua tulipotoka

Kutoka sitoki nimetekwa nyara Kukuwacha siwezi kibarua ngumu

Nashindwa ni nini ntafanya uridhike Nimetekwa ndani

Mtandao wa mapenzi Basi nakuomba
Uniteke tu bila mateso




Chorus

Tazama, nimezama Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai Kama wanipenda, jaribu kunipa raha

Verse 2

Mi nashangaa, watu wakisema

Eti tunapendana, japo tunazozana

Ni vizuri mami, nyumba kuwa na siri

Lakini jaribu, tusuluhishe

Bila hivyo, itakuwa mchezo

Wa kuigiza, kwenye mambo bandia

Mimi sitaki, mambo ya kujifanya

Ati tunapendana, tena tunatesana


Nimejaribu sana kujitoa ndani

Kila nikipanga napangua mwenyewe

Natamani sana ungeelewa hivyo

Mimi mateka Mimi pumbavu

Wa penzi lako Nieleze ni lini ntakuwa huru




Chorus

Tazama, nimezama

Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai

Kama wanipenda, jaribu kunipa raha



Verse 3

Jaribu baby

Mambo ya kunifanya kumbafu haifai

Mambo yo yo yo yo yo

Haifai

Jaribu baby, tusuluhishe


Nimejaribu sana kujitoa ndani

Kila nikipanga napangua mwenyewe

Natamani sana ungeelewa hivyo

Mimi mateka, mahabusu

Wa penzi lako

Nieleze ni lini ntakuwa huru



Chorus
Tazama, nimezama

Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele

Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai

Kama unanipenda, jaribu kunipa raha