Wednesday, 13 July 2016

NITAFANYA LYRICS BY KIDUM


Verse 1 [Kidum]

Ikiwa umeamua kunitoroka

Ikiwa unahisi hujiskii nami tena

Na mbona imekuwa ngumu kunidokeza

Naona ni bora nilie leo, badala ya kesho

Kupenda, usipende Ni kama kujitia kitanzi

Nitachimba na sururu Kwa ardhi nikitafuta penzi lako

Ni heri nipigwe fimbo kwa mwili

Sababu ntajikuna ama ntajikanda na maji moto

Maumivu ya penzi, mtu hajikuni

Wala hajikandi na maji, na hakuna upasuaji



Chorus

Kama Kuna kosa nimewahi fanya (nielezee)

Kama Kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi)

Na kama Kuna kitendo linaweza tendwa (nielezee)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Verse 2 [Lady Jay Dee]

Kweli hukumbuki ulioyafanya Ni kweli unakumbuka tulikotoka

Sisemi habari zozote za kusikia Bali kwa ushahidi niliouona

Msamaha mara ngapi Umeshaomba na bado

Chenye makosa mangapi Niliyoyafumbia macho

Mpaka leo nahisi kufika kikomo Maumivu yanazidi

Ndani ya moyo Sitaki kwenda mbali kwani uko moyoni

Nikusamehe mimi mara ngapi wee Nielezee mpenzi mara ngapi

Chorus

Unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu)

Ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho)

Je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia) Sitoweza (utaweza wee)

Nimechoka (usichoke) Nimeshindwa (usishindwe)

Naondoka (usiondoke) Sitoweza (utaweza yee)

Nimechoka Nimeshindwa (usishindwe)

Naondoka (usishindwe)



Verse 3

Ukihesabu mara ngapi umenisamehe Ni kama kuhesabu 

Ni mara ngapi mtoto kaharibu nappy Usichoke

Usiondoke Usilie Niko hapa kukulinda

Chorus

Kama Kuna kosa nimewahi fanya (nielezee)

Kama Kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi)

Na kam Kuna kitendo lingeweza tendwa (nielezee)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Nitafanya (fanya) Nitatenda (tenda)

Unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu)

Ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho)

Je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia)

Sitoweza (utaweza wee) Nimechoka (usichoke)

Nimeshindwa (usishindwe) Naondoka (usiondoke)

Sitoweza (utaweza yee) Nimechoka

Nimeshindwa (usishindwe) Naondoka (usishindwe)

No comments:

Post a Comment