Wednesday, 13 July 2016

MAPENZI LYRICS BY KIDUM


verse 1

Kama ni mapenzi Ya kuniudhi kila saa

Ya kunifanya mi kulia Na kama huridhiki

Na mbona hujasema Ili niweze rekebisha

Nifanye mambo shwari Nikiamini u kwangu

Na kukusifu kwa wazazi Hujali tenda hisia zangu

Sijui tunapokwenda Lakini najua tulipotoka

Kutoka sitoki nimetekwa nyara Kukuwacha siwezi kibarua ngumu

Nashindwa ni nini ntafanya uridhike Nimetekwa ndani

Mtandao wa mapenzi Basi nakuomba
Uniteke tu bila mateso




Chorus

Tazama, nimezama Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai Kama wanipenda, jaribu kunipa raha

Verse 2

Mi nashangaa, watu wakisema

Eti tunapendana, japo tunazozana

Ni vizuri mami, nyumba kuwa na siri

Lakini jaribu, tusuluhishe

Bila hivyo, itakuwa mchezo

Wa kuigiza, kwenye mambo bandia

Mimi sitaki, mambo ya kujifanya

Ati tunapendana, tena tunatesana


Nimejaribu sana kujitoa ndani

Kila nikipanga napangua mwenyewe

Natamani sana ungeelewa hivyo

Mimi mateka Mimi pumbavu

Wa penzi lako Nieleze ni lini ntakuwa huru




Chorus

Tazama, nimezama

Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai

Kama wanipenda, jaribu kunipa raha



Verse 3

Jaribu baby

Mambo ya kunifanya kumbafu haifai

Mambo yo yo yo yo yo

Haifai

Jaribu baby, tusuluhishe


Nimejaribu sana kujitoa ndani

Kila nikipanga napangua mwenyewe

Natamani sana ungeelewa hivyo

Mimi mateka, mahabusu

Wa penzi lako

Nieleze ni lini ntakuwa huru



Chorus
Tazama, nimezama

Ndani ya bahari, la penzi lako

Siwezi, kusonga mbele

Kurudi nyuma, sijielewi

Haya mapenzi ya fujo hayafai

Kama unanipenda, jaribu kunipa raha

No comments:

Post a Comment