Verse 1
Ukiona mwanaume kwa hali ya kulia, jua yakwamba ameguswa pahali
Hapo zamani nilidhani mwanaume akipoteza kazi ndio uchungu, ndio unyonge
Kumbe mapenzi ndio sumu kali, inayofanya mwanaume kulia
Kama mtoto mtoto, kama kidogoyo
Hapembelezwi, hanyamazishwi, machozi yake inatoka ikienda tumboni
Hapembelezwi, hanyamazishwi, machozi yake inatoka ikienda tumboni
Chorus
Mulika mwizi, mulika na tochi, mulika (mulika mwizi)
Mulika mwizi, kama kuna giza mulika
Nimulikie mwizi, nasumbuka, nataka kujua nani mwizi wa mapenzi
Barua pepe kwa simu ya rununu, ujumbe mfupi unafutwa na sekundi tatu (sekundi tatu)
Nilimpenda baibe wangu, nikampea roho yangu, amechukuliwa, amenyakuliwa
Jamaa fulani hapa mtaani, mwenye magari, na mapesa, amechukua baibe
Ikanifanya crazy,sipembelezwi, sinyamazishwi
Machozi yangu yanatoka yakienda tumboni
Msiomboleze, mnamujua huyu jamaa, kajifanya bubu, wengine vipofo
Chorus
Mulika mwizi, nimulikie mwizi
Nimulikie mwizi, nasumbuka, nataka kujua nani mwizi wa mapenzi
Nani mwizi wa mapenzi
Verse 3
[Sanaipei]
Ukiona baibe wako anaingia bafu na simu mkononi, huyo ni mwizi (mulika mwizi)
Uniona mzee wako anazima simu kila mara akiwa kwa nyumba, mulika mwizi (mulika mwizi)
Oh-o-o-o oh oh oh-o-o-o
Oh-o-o-o –o-o
Nimulikie mwizi jameni, (mulika mwizi)
Mulika mwizi, nionyeshe, niambie ni wapi
Nimulikie mwizi, mwizi wa mapenzi, mwizi wa mapenzi (mulika mwizi)
Nani mwizi wa mapenzi
Nani mwizi wa mapenzi (mulika mwizi)
Wani ua, wani umiza (oh –o-o-o-o)
Mulika na tochi, natazama mbele si nyuma
Mulika mwizi, kila mtu mwizi wa mapenzi, kila mtu mwizi wa mapenzi
Pia mimi mwizi wa mapenzi
No comments:
Post a Comment