Tuesday 28 November 2017

SIKOMI LYRICS BY DIAMOND PLATNUMZ


Wanasemanga mapenzi safari,
Unavyopita ndo jinsi unajongea
Ila niendako ni mbali sijui ka ntafika
Sababu natembea, niliposikia gabari

Yakisifika nikakesha nangojea ah
Akabariki Jalali na nikawika muziki



Nikauotea
Ile kumpaka maka
Nikajia ndio kwa gomo movi
Kumbe mapenzi hayataki haraka
Nikama Tango natia tu chumvi
Mwenzenu nikaoza haswa
Na kuitia kitandani mjuzi
Eti nataka fukuza paka
badala ya mbwa nikafuga mbuzi

mmh wivu ukanifanya nikagombana na marafiki
ugomvi na mamangu akiniambia siambiliki
moyo ukanambia Naseeb sasa mapenzi Basi
ila nang’ang’ania najaribu kuipinga nafsi
Esma ananambia mdogo wangu mapenzi basi



Ila nang’ang’ania
nikiumizwa na huyu kesho na mwingine

Ooh mboni sikomi sikomi sikomi
licha ya mateso haya
Najiuliza oh sikomi
Oh sikomi mbona (sikomi)
Mbona jamani sikomi
Licha ya mateso haya ah
Mmmmh

Aliyonifanyia wa central,
akia-mungu siyawezi sema
Ila nimejifunza kesho siwaamini wacheza sinema
Moyo walinipatia mateso
siwezi kumeza siwezi tema
mana sikushanga ile ghafla
toka CCM kwenda CHADEMA


wanasema kitanda ukitandika sharti ukikalie
nikajitia ukamanda yatakwisha
wacha nivumilie kila kiza kikitanda
ndo visa machozi mi nilie
penzi yakatia parapanda
kuwaita waje washambulie

aah acha na PENNY we darling
nilomuhongaga gari aliponambia ana mimba
mwisho wa siku akaichomoa chali
Molah akanitunuku ZARI
Akanizalia dume na mwali
Nilivomjinga nika-cheat aibu mpaka
Kwa vyombo vya habari

Moyo unanambia NASEEB sasa mapenzi basi
Ila nang’ang’ania najaribu kuipinga nafsi
LAIZER ananambia simba mapenzi basi
Ila nang’ang’ania nikiumizwa na huyu
Kesho na mwingine


Ooh mboni sikomi
Mboona sikomi
Mboona jamani sikomi
Licha ya mateso haya
Nishafumaniwa oh sikomi
Nikafumaniwa mimi sikomi
Nishapambana na watu (sikomi)
Licha ya mateso haya ah
Mateso mama


Ayo LAIZER
a

No comments:

Post a Comment