Tuesday, 19 July 2016

NITAREJEA LYRICS BY DIAMOND PLATINUMZ FT HAWA



Aah vipi mizigo umesha weka tayari mh aah sijechelewa nikaja achwa na gari mh aah

Basi jikaze usilie mpenzi aah mi nitarudi niombee kwa Mwenyezi aah
Zile taabu na njaa msimu mzima mavuno hakuna hua nakosa raha pale mkikosa cha kutafuna




Roho yangu inauma sema nitafanya nini na pesa sina nakuonea na huruma bora niende mjini kusaka tumaa

Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea wadanganye na vibagia waambie pipi nitawaletea

Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea na usichoke kuvumilia na kila siku kuniombea

Wewe unajua kwamba nafsi na roho vitakuwa na wasiwasi upweke na moyo utajawa na simanzi



Nitapo kuwa nakwenda shambani alafu niko peke yangu honey nitapo kuja kuwa na majirani nitaumia aah
Pale ninapotoka kisimani ama nipo na kuni kichwani sina wa kunitua nyumbani nitalia

Maneno yako yananifanya nakosa raha na mawazo hata mwenzako sijawahi kufika Dar huu ndo mwanzo

Vile nakwenda na sijui pa kukaa wala mavazi ooh we niombee niepushwe na balaa na maradhi ooh eeh



Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea wadanganye na vibagia waambie pipi nitawaletea

Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea na usichoke kuvumilia na kila siku kuniombea

Unapokwenda kama ukifika salama utukumbuke na sisi usisahau kwaba mkeo na wana umetuacha na dhiki

Hilo usijali ila naomba chunga sana ogopa na marafiki wakikulagai hata kwa mbegu za mtama waambie sidanganyiki




Unapokwenda kama ukifika salama utukumbuke na sisi kumbuka mkeo nyumbani na wana umetuacha na dhiki
Hilo usijali ila naomba chunga sana ogopa na marafiki wakikulagai hata kwa mbegu za mtama waambie sidanganyiki eeeh eeeh oooh nitarejea mama niombee nirudi salama oooh watoto wadanganye iih uuh uuh aah tozalee zijaee hmm kamaaa…



Kama watoto wakinililia waambie kesho nitarejea (nitarejea mama) wadanganye (uuh wadanganyee) na vibagia waambie pipi nitawaletea

Kama watoto wakinililia (kamaa)waambie kesho nitarejea (nitarejea mama) na usichoke kuvumilia (usichoke) na kila siku kuniombea (nirudi salama)

No comments:

Post a Comment