[Verse 1 – Professor Jay]
Niliacha kazi nifanye muziki wakatabiri nitalost
Wengine wakanishawishi tuloge kuondoa mikosi
Nakomaa na muziki ingawa jua la utosi
Naamini wote tunapita na kamwe maiti haijioshi
Jina langu lishatumika sana kutajirisha watu
Nyota ndogo alishasema kuna watu na viatu
Bunduki haiui watu ila watu ndio wanaua watu
Dunia kama jalala tazama kwa jicho la tatu
Ni saa mbaya watu wanahusda na roho mbaya
Tunawaita watakatifu kumbe ndio ma-vampire
Yalisemwa mengi demu wangu alivyotoroka
Ni fundisho tosha na changamoto kwa mwanachoka
Nimepita mengi mitihani ya kila namna
Ndio maana mi sishangai wakiniita mbeba lawama
Washkaji wengine fake kwenye deal hawakujui
Wanadhani kila jogoo akiwika ni asubuhi
Riziki hamuwezi iziba labda mtaichelewesha tuu
Mnakesha mnishushe Mwenyezi ananipaisha
Kote mlikobana kidume ndio natusua
Mnanijua, nakamua, roho za wanga zinaungua
Platnum!
Niliacha kazi nifanye muziki wakatabiri nitalost
Wengine wakanishawishi tuloge kuondoa mikosi
Nakomaa na muziki ingawa jua la utosi
Naamini wote tunapita na kamwe maiti haijioshi
Jina langu lishatumika sana kutajirisha watu
Nyota ndogo alishasema kuna watu na viatu
Bunduki haiui watu ila watu ndio wanaua watu
Dunia kama jalala tazama kwa jicho la tatu
Ni saa mbaya watu wanahusda na roho mbaya
Tunawaita watakatifu kumbe ndio ma-vampire
Yalisemwa mengi demu wangu alivyotoroka
Ni fundisho tosha na changamoto kwa mwanachoka
Nimepita mengi mitihani ya kila namna
Ndio maana mi sishangai wakiniita mbeba lawama
Washkaji wengine fake kwenye deal hawakujui
Wanadhani kila jogoo akiwika ni asubuhi
Riziki hamuwezi iziba labda mtaichelewesha tuu
Mnakesha mnishushe Mwenyezi ananipaisha
Kote mlikobana kidume ndio natusua
Mnanijua, nakamua, roho za wanga zinaungua
Platnum!
[Chorus – Diamond Platnumz]
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
[Verse 2 – Professor Jay]
Walishazusha nimekufa, eti nimepata ajali
Washindwe na walegee Mwenyezi niepushie mbali
Wakasema nina ukimwi kwa kuwa nilikonda ghafla
Wanataka kunizika mzima kabla sijafa
Waliosema nina ngoma wengine tushawafukia
Wanaoomba nife leo naamini watatangulia
Mama pumzika pema, daima tunakulilia
Na bado wanachonga sana, but man the king is here
Daima mtaji wangu ni nguvu zangu mwenyewe
Simwamini mtu kamwe najiamini mi mwenyewe
Hata nikinywa maji wanadai nakunywa pombe
Mi sijali, I knock them hard Mwanalizombe
Bado tu napambana kibarua kisiote nyasi
Daima sitawadhuru wale wote walioniasi
Nikikaa kimya msidhani sijasikia
Sio bahati sio ngekewa ni sauti iliyobarikiwa
Holla!
Walishazusha nimekufa, eti nimepata ajali
Washindwe na walegee Mwenyezi niepushie mbali
Wakasema nina ukimwi kwa kuwa nilikonda ghafla
Wanataka kunizika mzima kabla sijafa
Waliosema nina ngoma wengine tushawafukia
Wanaoomba nife leo naamini watatangulia
Mama pumzika pema, daima tunakulilia
Na bado wanachonga sana, but man the king is here
Daima mtaji wangu ni nguvu zangu mwenyewe
Simwamini mtu kamwe najiamini mi mwenyewe
Hata nikinywa maji wanadai nakunywa pombe
Mi sijali, I knock them hard Mwanalizombe
Bado tu napambana kibarua kisiote nyasi
Daima sitawadhuru wale wote walioniasi
Nikikaa kimya msidhani sijasikia
Sio bahati sio ngekewa ni sauti iliyobarikiwa
Holla!
[Chorus – Diamond Platnumz]
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
[Verse 3 – Professor Jay]
Mungu walaze pema waliosemwa wakajiua
Ingawa wote tunapita naamini Maisha ni hatua
Maneno ya watu sumu, yanaponya na yanaua
Please nipe ujasiri mpaka siku ukinichukua
Wape nguvu wale wote waliokata tamaa
Maneno yanaleta hila na mzozo kwenye mitaa
Wanahesabu mabaya tuu na mema hawayaoni
Wanakuchekea machoni, wanakuroga moyoni
Wanacheka chinichini wakati una msiba
Wa kwanza kukutangaza kwa watu ukiwa na shida
Wanatamani wapangue kila Mola alichopanga
Wanatangaza Amani huku wameficha mapanga
Mungu walaze pema waliosemwa wakajiua
Ingawa wote tunapita naamini Maisha ni hatua
Maneno ya watu sumu, yanaponya na yanaua
Please nipe ujasiri mpaka siku ukinichukua
Wape nguvu wale wote waliokata tamaa
Maneno yanaleta hila na mzozo kwenye mitaa
Wanahesabu mabaya tuu na mema hawayaoni
Wanakuchekea machoni, wanakuroga moyoni
Wanacheka chinichini wakati una msiba
Wa kwanza kukutangaza kwa watu ukiwa na shida
Wanatamani wapangue kila Mola alichopanga
Wanatangaza Amani huku wameficha mapanga
[Chorus – Diamond Platnumz]
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele basi nishike mkono nishinde
Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwenye hii vita milele mwanachoka daima Nishinde
No comments:
Post a Comment